DALILI ZA MWANAUME ANAYEKUPENDA - Bongo Loves

DALILI ZA MWANAUME ANAYEKUPENDA

Read More

Image result for warembo
DALILI ZA MWANAUME ANAYEKUPENDA
(1)       ANAKUTAZAMA MARA KWA MARA
Mara nyingi wanaume huanzisha hisia zao za kimapenzi kwa kutumia macho yao na hivyo uonapo mwanaume anakutazama mara kwa mara na macho yenu yanagongana anageuza kichwa ujue tayari ameanza kuona uthamani wako kama mpenzi.
(2)       ANAJIVUTA KARIBU NAWE
Uonapo mwanaume anatafuta kila sababu ya kutaka kuongea nawe mara kwa mara ni dalili ya kwamba anapenda uwe sehemu ya maisha yake.Simu za mkononi inaweza kuwa chombo muhimu sana katika eneo hili.
(3)       ANAKUFAGILIA SANA
Mwanaume anapokuwa ameona mwanamke ambaye anatamani awe mpenzi wake na mwishowe awe mke ataanza tabia ya kumsifia mwanamke huyo sio hilo tu bali pia atajitahidi kumtia moyo mwanamke huyo kumsogeza mahali ambapo mwanamke atajiona kuwa ni wa muhimu na anaestahili mema na mafanikio.Hivyo basi  kumfanya mwanamke huyo kuhusisha mafanikio yake na mtu ambaye amekuwa akimtia moyo na kumwona kuwa anaweza kushinda vikwazo vyovyote vile.
(4)       MTOA ZAWADI
Mwanaume anaekupenda atajitahidi kukutafutia zawadi nzuri wakati ambapo hakuna tukio lolote la kisherehe. Kwa kufanya hivyo anamuonyesha mwanamke kuwa yuko ndani ya moyo wake na ni wa muhimu kwake.
(5)       MNATOKA KWA KIWANGO KIKUBWA
Mwanaume anayependa mwanamke atajitahidi kumtoa mpenzi wake kwenda nae katika hoteli nzuri au maeneo ya starehe yenye hadhi kubwa. Mwanaume huyo hataangalia gharama za hayo yote na mwanamke aonyeshapo kuwa haoni umuhimu wa matumizi makubwa mwanaume huyo atapuuzia kabisa maneno yote. Mwanaume huyo ataonekana kutokujali muda mnaokuwa pamoja na hatakuwa na haraka ya kuondoka.
(6)       HASHOBOKI
Mwanaume ambae anakupenda atajitahidi sana asiwe anakodolea macho wanawake wengine (hashobokei wanawake wengine na hana time na vicheche). Asilimia kubwa ya wanaume wana udhaifu wa kukodolea macho wanawake wengine hata wakiwa na wapenzi wao. Lakini mwanaume anayemheshimu mpenzi wake atajitahidi sana kujizuia hali hiyo isiendelee au kuonekana awapo na mpenzi.
(7)       ANAKUPENDELEA
Mwanaume anapompenda mwanamke atajikuta kuwa anaanza kumpa kipaumbele mwanamke aliemchagua. Anaweza asiwe na pesa lakini akiona mpenzi wake anahitaji jambo fulani atafanya juu chini amtimizie haja yake. Mara nyingine hali hii ikiwa kubwa mwanaume huyu anaweza kusahau hata wazazi na ndugu zake. Mwanaume huyo atajikuta anaacha mambo yaliyokuwa muhimu kwake kuwa na mwanamke aliemchagua. Atakusaidia hata kabla hujaomba msaada kwake.
(8)       ANATAFUTA MIZIZI YAKO
Mwanaume anapompenda mwanamke na kutamani kuwa sehemu ya maisha yake ataonekana kupenda kujua mengi juu ya familia na ndugu za mwanamke aliemchagua. Mwanamke aonapo maswali ya aina hiyo yanarudiwa ajue kuwa mwanaume huyo anampenda na anatafuta uhakika wa ubora wa familia ya mke wake mtarajiwa.
(9)       ANAKUCHUNGA KWA FIMBO YA WIVU
Wivu sio kitu kibaya pale ambapo lengo lake ni kulinda kitu unachokithamini sio hilo tu bali pale uonapo wivu wake haukunyimi uhuru wako. Mwanamke aonapo mpenzi wake ameanza tabia ya kuuliza “Uko wapi”? “Utarudi home saa ngapi”? “Mbona nasikia kelele  uko wapi na unafanya nini huko”? Maswali yanayofanana na hayo yanaashiria kuwa moyoni mwake tayari amekufanya sehemu ya thamani ya maisha yake.
(10)   ANACHEKACHEKA OVYO
Uonapo mwanaume anacheka mara kwa mara awapo nawe tambua kuwa ameanza kukolea penzi. Mwanaume anapopenda anajikuta anafurahishwa na vitu vidogo vidogo asemavyo au afanyavyo mwanamke aliemchagua. Hali hii inaoneysha ni jinsi gani anamwona mwanamke huyo kuwa chanzo kizuri cha furaha maishani mwake.
(11)   ANAANZA KUKUNADI
Mwanaume aonapo kuwa sasa penzi lake kwa mwanamke aliempenda limekomaa ataanza kumtambulisha kwa marafiki zake na mbwembwe hizo zinaweza kuwagusa hata wazazi na ndugu zake wa karibu.
(12)   ANAPENDA KUKUGUSAGUSA
Mwanaume anapokuwa amependa atajikuta anataka kuimarisha mshikamano kati yake na mwanamke aliemchagua. Kwa kumshika mkono, kumkumbatia au kumvuta karibu yake wawapo kati ya watu wengi ni ishara ya kuonyesha kuwa sasa hataki mwanamke huyo atoke maishani mwake.Hilo ni tangazo la siri kwa wanaume wengine kusema vicheche chezeni mbali.
(13)   ATAKUIMBIA WIMBO UUPENDAO
Wanawake wengi wanapenda kusikia mwanaume akisema mara kwa mara kuwa anampenda. Kwa mwanaume aliyempenda kweli kweli atakuwa na urahisi wa kusema “Nakupenda mpenzi” mara kwa mara. Wimbo huu ni wa muhimu sana.N muhimu kuuchukulia kama ishara muhimu kwani Biblia inasema “Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi wake na wao waupendao watakula matunda yake. Apataye mke apata kitu chema naye ajipatia kibali kwa BWANA (MITHALI 18:21-22).
(14)   ANAKUHANGAIKIA
Mwanaume apendaye mwanamke atajitahidi kuhangaika juu ya mahitaji ya mwanamke aliemchagua utaona anakuwa makini hata kwa mahitaji madogomadogo mnapokuwa mmeachana.Utakuta anamuuliza mwanamke iwapo anahitaji hiki au kile.
(15)   ANAJIRUDI KWA UPOLE
Katika mapenzi hali ya kutoelewana haiepukiki kabisa na mwanaume ambaye anampenda mwanamke aliemchagua atatambua umuhimu wa kuomba msamaha pale anapokosea. Hata ikitokea mkagombana haichukui muda mrefu kwa yeye kuanza kubembeleza ili kurudisha hali ya amani. Vile vile mwanaume huyo ataonyesha heshima kwa kuepuka lugha ya matusi au dharau ya aina yoyote ile. Hii ni moja kati ya dalili kubwa ya penzi lenye nguvu.
(16)   ANAJINADI KWA NDUGU ZAKO
Mwanaume mwenye nia ya kumfanya mwanamke awe sehemu ya maisha yake ataanza kufanya mambo ambayo ndugu na marafiki wa mwanamke watamwona kuwa ni mtu wa maana na mwenye thamani. Mwanaume huyo atafanya hayo kwani anajua kuwa furaha ya ndugu na marafiki zake itakuwa ni furaha ya mwanamke ampendae.
(17)   ANAFANYA BIDII KITANDANI
Asilimia kubwa ya wanaume wana matatizo ya nguvu za kiume na kuwahi kumaliza lakini pamoja na matatizo hayo mwanaume ambaye amempenda mwanamke aliemchagua atahangaika kutafuta njia mbalimbali za kuhakikisha kuwa mwanamke alie nae kitandani anaridhika kabisa. Hiki ni kipengele muhimu sana cha kuangalia kwani sayansi ya mapenzi imethibitisha kuwa asilimia kati ya 80 na 85 ndoa huingia katika migogoro kutokana na kukosekana utamu wa kutosha katika tendo la ndoa katika Biblia kitabu cha KUMBUKUMBU LA TORATI inaonyeshwa kuwa ni wajibu wa mwanaume kumfurahisha mwanamke. “ mtu atwaapo mke mpya asiende vitani pamoja na jeshi, wala asipewe shughuli juu yake yoyote akae faragha mwaka mmoja nyumbani mwake apate mfurahisha mke aliyemtwaa (Kumbukumbu la Torati 24:5) kutokana na agizo hilo toka kwenye Biblia utaona kuwa mwanaume ambaye anashindwa kumfurahisha mwanamke katika eneo hilo anampa haki mke wake amdharau kama Biblia kwa mara nyingine tena inavyoonyesha”.
“Maji mengi hayawezi kuzimisha upendo wala mito haiwezi kuzimisha kama mwanaume angetoa badala ya upendo mali zote za nyumbani mwake. Angedharauliwa kabisa” (Wimbo uliobora 8:7).
ULAZIMA WA KUFANYA MABADILIKO KATIKA MAPENZI
Ukweli ni kwamba kila mtu angependa furaha ya mapenzi aliyoanza nayo iendelee kudumu lakini kwa wengi hiyo ni historia ya mbali na kwa wengine wanaona kuwa jambo hilo la kuendeleza furaha siku zote haliwezekani toka nianze kazi yangu ya ushauri na vipindi redioni nimekuwa nikikutana na kesi nyingi sana za kusikitisha na kuumiza moyo na sio hilo tu bali hata mimi mwenyewe nimekutana na changamoto kubwa ambazo zimenifanya niendelee kufanya utafiti zaidi kutafuta siri ya uhusiano wenye furaha ya kudumu.
Katika sura hii nitaonyesha mwanga niliouona na katika sura ifuatayo nitaonyesha moja kati ya njia kuu muhimu ya kudumisha furaha katika mahusiano ya kimapenzi. Ugunduzi huu ni wa kisayansi na naona kuwa ni moja kati ya ufunguo muhimu sana katika mahusiano ya kimapenzi mwanadamu ameumbwa aweze kuishi kwa furaha wakati wote jambo ambalo linaimarisha kinga ya mwili dhidi ya maradhi na kusababisha akili kufanya kazi vizuri zaidi. Ili kudumisha  furaha na amani mwanadamu ameumbwa na uwezo wa kurudia katika kiwango kile kile cha furaha alichokuwa nacho mwanzoni bila kujali kama mtu huyo amekutana na mambo mazuri au mabaya. Hali hii hutokea kwani mwanadamu hujikuta anayazoea mabadiliko yanayomkuta yawe mazuri au mabaya ili kudumisha kiwango kile kile cha furaha au amani. Hali hii kitaalamu huitwa HEDONIC ADAPTION na kuna mifano inayoweza kukuonyesha jinsi gani hata wewe mwenyewe umekumbana na hali hiyo.
(1)        Unanunua saa mpya ya ukutani na unaiweka nyumbani na mwanzoni unasikia mlio wa saa inapotembea lakini baada ya muda fulani unapokuwa umezoea mlio huo unajikuta huusikii kabisa.
(2)        Mtu ambaye anahamia kwenye nyumba uliopo kando ya barabara ambapo magari mengi hupita mwanzoni anasumbuliwa na kelele za magari lakini baada ya muda fulani anaizoea hali hiyo na kuwa na amani tele na wala hasumbuliwi na kelele za magari kama mwanzoni.

Related Posts

0 Response to " DALILI ZA MWANAUME ANAYEKUPENDA"

Post a Comment